• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

Bashungwa Aweka Mawe ya Misingi kwa Miradi ya Maendeleo Mkoani Pwani

Posted on: October 9th, 2024

Waziri wa Ujenzi, Mhe. Innocent Bashungwa, akiwa ameambatana na Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Abubakar Kunenge, amezindua miradi mbalimbali ya maendeleo na kuweka mawe ya msingi kwa miradi hiyo, ikiwemo shule za sekondari, masoko ya kisasa, hospitali, na nyumba za watumishi. Hii ni sehemu ya ziara yake ya kikazi ya kukagua maendeleo ya miradi mkoani Pwani.

Katika siku ya pili ya ziara hiyo, Mhe. Bashungwa alitembelea Halmashauri ya Mji Kibaha, Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha DC, na Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze. Alifanya uwekaji wa mawe ya msingi katika shule tano za sekondari, ambapo mbili ziko katika Halmashauri ya Kibaha Mji, moja katika Halmashauri ya Kibaha DC, moja katika Halmashauri ya Chalinze, na nyingine katika Halmashauri ya Bagamoyo.

Aidha, Waziri Bashungwa aliweka mawe ya msingi katika masoko mawili, Soko la Kisasa la Mlandizi na Soko la Bwilingu, yaliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze. Pia, alizindua rasmi ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Kibaha DC pamoja na nyumba nane za watumishi katika Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze.

Baada ya uwekaji wa mawe ya msingi kwa miradi hiyo, Mhe. Bashungwa alitatua changamoto kadhaa zilizokuwa zinakwamisha miradi hiyo, ikiwemo barabara na upatikanaji wa maji katika maeneo husika.

Waziri Bashungwa alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, kwa kutenga trilioni 1.3 kwa ajili ya maendeleo ya mkoa wa Pwani. Alimpongeza pia Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Abubakar Kunenge, kwa usimamizi thabiti wa utekelezaji wa miradi hiyo, ambayo inaendana na Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Katika mikutano ya hadhara aliyoifanya na wananchi, Waziri Bashungwa aliwahamasisha kujitokeza kwa wingi kujiandikisha katika daftari la wapiga kura, ili waweze kuchagua viongozi sahihi katika uchaguzi ujao.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC Kunenge Ashiriki Kupiga Kura , Awataka Wananchi wa Pwani kuendelea kujitokeza kwa wingi

    October 29, 2025
  • Dumisheni Umoja na Utulivu kuelekea Uchaguzi Mkuu- Kamati ya Amani Pwani

    October 28, 2025
  • Vituo 3,941 vya kupiga kura vyaandaliwa Mkoani Pwani Kuelekea Uchaguzi mkuu

    October 27, 2025
  • RC Kunenge akabidhi Vitendea kazi vya Zaid ya Sh. Bilion 7 kwa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Pwani

    October 24, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.

  • Situs Toto
  • Situs Slot Gacor
  • AXL777
  • Situs Toto
  • AERO88
  • Situs Slot Gacor
  • DORA77
  • DORA77
  • DORA77
  • Toto Togel
  • Situs Toto
  • AXL777
  • AERO88
  • Situs Slot Gacor
  • Situs Slot Gacor
  • Situs Toto
  • Toto Slot Gacor
  • Toto Slot
  • Toto Slot
  • DORA77
  • KOI200
  • KOI200
  • SILVAWIN
  • AXL777
  • YAMITOTO
  • NABITOTO
  • YAMITOTO
  • KOI200
  • KOI200
  • KOI200