Katibu Tawala wa Mkoa wa Pwani, Pili Mnyema, , ametembelea na kukagua miradi miwili mikubwa yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 1.9 Miradi hiyo ni ujenzi wa jengo la ofisi ya Halmashauri ya Mji Bagamoyo litakalogharimu kiasi cha shilingi Bilion 1.8 pamoja na mradi wa ukarabati wa Soko la Uhindini unaogharimu takribani shilingi milioni 105.7
Katika ziara hiyo ya kikazi katika Halmashauri ya Bagamoyo, Mnyema pia alizungumza na watumishi wa halmashauri hiyo ambapo aliwataka kufanya kazi kwa weledi na kwa kuzingatia taratibu, sheria na kanuni za Utumishi wa Umma.
“Tufanye kazi kwa weledi na uadilifu kwa kuzingatia sheria. Tumepewa jukumu kubwa la kutoa huduma bora kwa wananchi, hivyo hatuna budi kulitekeleza. Tujiepushe na yale yaliyokatazwa,” alisema Mnyema.
Mnyema amewataka watumishi hao kuwa na upendo kazini na kuacha tabia ya kutengenezeana majungu.
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani
Sanduku la Posta: 30080 Kibaha
Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500
Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500
Barua pepe: barua@pwani.go.tz
Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.