• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

Mkenda awataka Wazazi na walenzi waliokumbwa na mafuriko Kibiti na Rufiji kuhakikisha watoto wao wanasoma shule zilizokaribu na maeneo waliyohamia

Posted on: April 22nd, 2024

Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Profesa Adolf Mkenda ametoa maagizo kwa Wazazi na walezi ambao wamekumbwa na mafuriko katika maeneo mbalimbali Wilayani Kibiti na Rufiji kuhakikisha watoto wao wanasoma shule zilizokaribu na maeneo waliyohamia.

Aidha amewaelekeza walimu kuwapokea wanafunzi waliotoka maeneo ya mafuriko bila masharti na kutoa taarifa kwa Maafisa elimu Ili kupata idadi kamili ya waliorudi shuleni.

Pro.Mkenda ametoa maagizo hayo April 22, 2024 alipokuwa katika ziara ya siku moja Wilaya ya Rufiji na Kibiti kukagua shule zilizoathirika na mafuriko, kutembelea makambi pamoja na kutoa vitabu na daftari kwa wanafunzi waliokumbwa na mafuriko

Amesema lengo la Serikali ni kuhakikisha wanafunzi waliokuwa kwenye maeneo ya mafuriko wanaendelea na masomo popote walipo wakati taratibu nyingine zikiendelea za kuboresha miundombinu maeneo ambayo hayana mafuriko

" Mwanafunzi akija kwenye shule yako mpokee mengine yatatatuliwa baadae haya ni maelekezo walimu wote wayasikie, Rais Samia Suluhu Hassan ameagiza tuongezee nguvu kuhakikisha wanafunzi kwenye maeneo yaliyoathiriwa wanaendelea na masomo," amesema.

Mkuu wa Mkoa wa PWANI Abubakar Kunenge amesema katika maeneo yaliyoathiriwa na mafuriko watazungumza na wananchi na maamuzi ya Serikali yatafanyika kunusuru maisha yao kwa kuhamia sehemu salama.

Kunenge amesema baada ya mafuriko kipaumbele kiliwekwa kwa wanafunzi ambao wanatarajiwa kufanya mitihani mwaka huu na kutafutiwa shule kwa haraka na sasa wanafunzi wengine wanaendelea kurejea mashuleni kwenye maeneo ambayo wanaishi.

Afisa elimu Mkoa wa Pwani Sara Mlaki ameeleza kwamba katika Wilaya ya Rufiji wanafunzi 7,264 wameathiriwa na mafuriko huku Wilaya ya Kibiti wanafunzi 824 wakikumbwa na adha hiyo.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC Kunenge Ashiriki Kupiga Kura , Awataka Wananchi wa Pwani kuendelea kujitokeza kwa wingi

    October 29, 2025
  • Dumisheni Umoja na Utulivu kuelekea Uchaguzi Mkuu- Kamati ya Amani Pwani

    October 28, 2025
  • Vituo 3,941 vya kupiga kura vyaandaliwa Mkoani Pwani Kuelekea Uchaguzi mkuu

    October 27, 2025
  • RC Kunenge akabidhi Vitendea kazi vya Zaid ya Sh. Bilion 7 kwa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Pwani

    October 24, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.

  • Situs Toto
  • Situs Slot Gacor
  • AXL777
  • Situs Toto
  • AERO88
  • Situs Slot Gacor
  • DORA77
  • DORA77
  • DORA77
  • Toto Togel
  • Situs Toto
  • AXL777
  • AERO88
  • Situs Slot Gacor
  • Situs Slot Gacor
  • Situs Toto
  • Toto Slot Gacor
  • Toto Slot
  • Toto Slot
  • DORA77
  • KOI200
  • KOI200
  • SILVAWIN
  • AXL777
  • YAMITOTO
  • NABITOTO
  • YAMITOTO
  • KOI200
  • KOI200
  • KOI200