• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Afunga kambi ya matibabu ya Macho,apongeza Ushirikiano wa Wadau

Posted on: December 9th, 2024

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Abubakar Kunenge, amehitimisha rasmi kambi ya matibabu ya macho iliyodumu kwa siku tatu, ikiwa na lengo la kutoa huduma za afya kwa wananchi wa Mkuranga. Kambi hiyo ilitoa huduma za utoaji wa miwani, dawa za macho, ushauri wa kitaalamu, pamoja na upasuaji wa mtoto wa jicho.

Huduma hizo zilitolewa na madaktari bingwa kutoka Hospitali ya Bilal Muslim Mission of Tanzania kwa kushirikiana na Beta Charitable Trust (UK), Kampuni ya Mawasiliano ya Tigo, na Mbunge wa Jimbo la Mkuranga, Mhe. Abdallah Hamis Ulega. Kambi hiyo ilifanyika katika Shule ya Msingi Mkuranga na Shule ya Msingi Kizapala, ikiwafikia mamia ya wananchi wenye mahitaji ya huduma za macho.

Akizungumza wakati wa kufunga kambi hiyo leo, Desemba 9, 2024, Mhe. Kunenge aliishukuru taasisi ya Bilal Muslim Mission of Tanzania kwa kutoa huduma bure kwa wakazi wa Mkoa wa Pwani, hususan katika Wilaya za Bagamoyo na Mkuranga. Alitoa wito kwa taasisi hiyo kuendelea kushirikiana na serikali ili kufikisha huduma hizi muhimu katika wilaya nyingine za mkoa huo.

Aidha, Mhe. Kunenge alitoa shukrani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuweka mazingira wezeshi yanayoruhusu taasisi binafsi kushirikiana na serikali katika kuboresha maisha ya wananchi. Pia alimpongeza Mhe. Abdallah Hamis Ulega kwa mchango wake katika kufanikisha kambi hiyo, huku akimshukuru Rais kwa kumteua Mhe. Ulega kuwa Waziri wa Ujenzi.

Kambi hii ni mfano wa mafanikio ya ushirikiano kati ya serikali, sekta binafsi, na wadau wa maendeleo katika kuhakikisha huduma za msingi za afya zinawafikia wananchi wengi zaidi.


Matangazo

  • No records found
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC Kunenge Ashiriki Kupiga Kura , Awataka Wananchi wa Pwani kuendelea kujitokeza kwa wingi

    October 29, 2025
  • Dumisheni Umoja na Utulivu kuelekea Uchaguzi Mkuu- Kamati ya Amani Pwani

    October 28, 2025
  • Vituo 3,941 vya kupiga kura vyaandaliwa Mkoani Pwani Kuelekea Uchaguzi mkuu

    October 27, 2025
  • RC Kunenge akabidhi Vitendea kazi vya Zaid ya Sh. Bilion 7 kwa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Pwani

    October 24, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.