• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

Mvua kubwa, Ufunguzi wa Mageti Bwawa la umeme Chanzo cha Mafuriko Bonde la Mto Rufiji

Posted on: March 15th, 2024

Madhara yaliyotokea kwa baadhi ya wakazi wanaoishi na kuendesha shughuli zao kando ya mto Rufiji yametokana na mto huo kujaa maji kufuatia mvua zilizonyesha hivi karibuni pamoja na maji yaliyotoka katika Bwawa la kufua umeme la Mwalimu Julias Nyerere.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge alipokutana na kuzungumza na waandishi wa habari ofisini kwake juu ya suala hilo Machi 14, 2024.

Katika ufafanuzi wake, Kunenge amesema kutokana na mvua hizo bwawa hilo lilijaa maji na kufikia kina cha mita za ujazo 183.85 ambayo wataalamu walifikia maamuzi kuwa baadhi ya mageti yafunguliwe ili kuruhusu maji hayo kupungua ambayo kwa sasa yamefikia mita za ujazo 183.45.

Amesema kabla ya kufunguliwa mageti hayo, Serikali ilitoa taarifa kwa wananchi kwa kutumia njia mbalimbali za kimawasiliano ikiwemo kutangaza katika Redio ya Rufiji FM, nyumba za ibada na hata kupitia wenyeviti wa vjiji na vitongoji ili waweze kuchukua tahadhari dhidi ya madhara ambayo yangeweza kutokea na wengine walitii wakaondoka na hata kuokoa mazao yao.

"Baada ya mageti hayo kufunguliwa katika bwawa hilo, maji yamesambaa katika bonde la mto Rufiji na kuleta mafuriko ambayo yamesababisha kuwepo kwa athari kwa wananchi wanaofanya shughuli za kilimo pembezoni mwa mto huo," amesema.

Ameongeza kuwa "athari mojawapo iliyopatikana ni kuharibiwa kwa mazao baada ya kufunikwa na maji mengi, hata hivyo wengine walifanikiwa kuokoa mazao yao kwa kuwa waliwahi kuondoka mara baada ya kupewa taarifa juu ya kufunguliwa kwa maji hayo.

Kuhusu usalama wa wananchi katika eneo hilo, Kunenge amesema tayari vyombo vya uokoaji vimefanyakazi na sasa hali inaendelea vizuri na akasisiti kuwa tahadhari lazima ichukuliwe kwa kuwa mvua kubwa zinatarajiwa kuendelea kunyesha.

“Tunaendelea kutoa elimu na tahadhari kwa wananchi kuwa waondoke katika maeneo hayo ili kuepusha vifo kwakuwa mvua nyingi zinatarajiwa kuendelea kunyesha hivyo kufanya mto Rufiji kuendelea kujaa maji,” amesema.

Mkuu huyo wa mkoa amefafanua pia kuwa kamati ya maafa inaendelea kufanya tathmini katika maeneo yote ya Wilaya za Rufiji na Kibiti ili kuweza kujua athari iliyopatikana na kuitolea taarifa kwa wananchi.

Bwawa la kufua umeme la Mwalimu Julias Nyerere tayari limeanza kuzalisha megawati 235.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC Kunenge Ashiriki Kupiga Kura , Awataka Wananchi wa Pwani kuendelea kujitokeza kwa wingi

    October 29, 2025
  • Dumisheni Umoja na Utulivu kuelekea Uchaguzi Mkuu- Kamati ya Amani Pwani

    October 28, 2025
  • Vituo 3,941 vya kupiga kura vyaandaliwa Mkoani Pwani Kuelekea Uchaguzi mkuu

    October 27, 2025
  • RC Kunenge akabidhi Vitendea kazi vya Zaid ya Sh. Bilion 7 kwa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Pwani

    October 24, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.