• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

Pwani Kuendelea Kulipa malimbikizo ya madeni ya Wastafu.

Posted on: June 23rd, 2023

Serikali ya Mkoa wa Pwani imesema itaendelea kulipa malimbikizo ya madeni ya watumishi waliostaafu na waliopoteza maisha wakiwa kazini kadri ya makusanyo ya mapato ya ndani yatakavyopatikana.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge leo Juni 22, 2023 kwenye kikao cha baraza la madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha maalum kilichoketi kujadili hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali - CAG.

Amesema anatambua uwepo wa madai ya watu katika Halmashauri za mkoa huo na kwamba hatua mbalimbali zimeendelea ili kuhakikisha wastaafu wote wanalipwa stahiki zao.

Amefafanua kuwa kwa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha, tayari wastaafu wameanza kulipwa kupitia vyanzo mbalimbali vya mapato kikiwemo cha fedha zitokanazo na mauzo ya viwanja ambapo kilitolewa kiasi ili kulisaidia kundi hilo.

“Natambua kuna wastaafu wanazidai halmashauri zetu, hatuwezi kumaliza kwa wakati mmoja madeni haya lakini tunachokifanya ni kutumia vyanzo vyetu vya mapato ya ndani kupunguza madeni haya, niwaombe watumishi muendelee kuwa wabunifu na kuanzisha vyanzo vingine vya mapato ili kushughulikia vikwazo kama hivi,” amesema Kunenge.

Awali, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha, Butamo Ndalahwa, aliliambia baraza la madiwani kuwa suala la madai ya watumishi wastaafu limekuwa likiwaumiza kichwa na kwamba wanaendelea kupambana kuhakikisha wanalipa stahiki za watu hao.

Ameongeza kuwa madai hayo yamedumu kwa muda mrefu hali inayosababisha kila mwaka kwenye ripoti ya - CAG kuingia kwenye hoja hivyo wanatamani kukamilisha.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC Kunenge Ashiriki Kupiga Kura , Awataka Wananchi wa Pwani kuendelea kujitokeza kwa wingi

    October 29, 2025
  • Dumisheni Umoja na Utulivu kuelekea Uchaguzi Mkuu- Kamati ya Amani Pwani

    October 28, 2025
  • Vituo 3,941 vya kupiga kura vyaandaliwa Mkoani Pwani Kuelekea Uchaguzi mkuu

    October 27, 2025
  • RC Kunenge akabidhi Vitendea kazi vya Zaid ya Sh. Bilion 7 kwa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Pwani

    October 24, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.