• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

Pwani yatarajia kutoa chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi kwa wasichana wasiopungua 18,823.

Posted on: April 25th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Pwani ,Mhandisi Evarist Ndikilo,ametoa onyo kwa mtu atakaejaribu kuzuia watoto ,kupata chanjo ya kuzuia saratani ya mlango wa kizazi, ambapo zoezi hilo linatarajiwa kuzinduliwa kimkoa april 30 mwaka huu .


Aidha ameeleza saratani hiyo ndiyo inayoongoza kwa kuua wanawake wengi ukilinganisha na saratani nyingine Tanzania,hivyo kuna umuhimu wa kuzuia ugonjwa huo kwa watoto hao.


Akifungua mkutano wa wadau wa chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi Mkoani Pwani, Mhandisi Ndikilo alisema kuwa , wazazi na walezi wahakikishe watoto wa kike waliofikisha miaka 14 wanaenda katika vituo vya kutolea huduma za chanjo ikiwemo vituo vya afya kwa ajili ya kupaiwa chanjo hiyo.


“Kamwe asiwepo mtu wa kuzuia watoto wetu ambao ni Taifa la Leo na Kesho kupata kinga hii muhimu ili kuepuka madhara makubwa yanayoweza kuwapata hapo baadae”alisisitiza Ndikilo.


Hata hivyo aliwahakikishia wananchi kuwa chanjo hiyo ni salama na haina madhara yoyote kwa walengwa ,kwani hutolewa na wataalamu wenye uzoefu mkubwa waliobobea katika fani hiyo .


Mhandisi Ndikilo aliwataka wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa halmashauri kusimamia utekelezaji wa zoezi hilo ili serikali ipate matokeo chanya na makubwa katika kukabiliana na tatizo hilo.


Alisema kuwa,Serikali imeamua kuanza kutoa chanjo hiyo,”: na nichukue fursa hii kuipongeza wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii ,Jinsia ,Wazee na Watoto kwa kushirikiana na wadau mbalimbali katika jitihada za kuboresha afya ya mabinti nchini ikiwa ni pamoja na kupunguza vifo vitokanavyo na saratani kwa kuanzisha chanjo dhidi ya saratani hiyo".


Aidha aliwaomba viongozi wa dini na viongozi mbalimbali kusaidia kupeleka ujumbe kupitia mihadhara na mikutano juu ya uanzishwaji wa chanjo hiyo.


Nae mratibu wa afya ya uzazi na mtoto mkoani humo ,Bi.Joyce Gordon alisema akinamama wengi ambao wapo kwenye hatari ya kuugua kansa ni wale wenye virusi vya ugonwja wa UKIMWI.


Pamoja na hilo,alisema wagojwa walioingiakatika Hospitali ya  Ocean road tangu mwaka 2006 -2016 ,inaonekana kansa inayoongoza ni ya mlango wa kizazi.


Bi.Joyce alielezea kuwa, takwimu za mwaka 2006 saratani hiyo ilikuwa ikiongoza ikifuatiwa na saratani ya matiti.

Alisema makisio ya ukubwa wa tatizo kwa mwaka 2002 yalikuwa ni zaidi ya 7,000 ambapo ikifikia 2025 makisio yanatarajia kufikia 12,416 hivyo inaonyesha tatizo kuzidi kukua.

Kwa upande wake mratibu wa chanjo mkoani Pwani,Abbas Hincha aliweka bayana kuwa walengwa wa chanjo hiyo kwa mwaka huu ni wasichana wote wenye miaka 14.


Hincha alisema wanatarajia kutoa chanjo kwa wasichana wasiopungua 18,823 katika mkoa huo

Matangazo

  • No records found
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC Kunenge Ashiriki Kupiga Kura , Awataka Wananchi wa Pwani kuendelea kujitokeza kwa wingi

    October 29, 2025
  • Dumisheni Umoja na Utulivu kuelekea Uchaguzi Mkuu- Kamati ya Amani Pwani

    October 28, 2025
  • Vituo 3,941 vya kupiga kura vyaandaliwa Mkoani Pwani Kuelekea Uchaguzi mkuu

    October 27, 2025
  • RC Kunenge akabidhi Vitendea kazi vya Zaid ya Sh. Bilion 7 kwa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Pwani

    October 24, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.

  • Situs Toto
  • Situs Slot Gacor
  • AXL777
  • Situs Toto
  • AERO88
  • Situs Slot Gacor
  • DORA77
  • DORA77
  • DORA77
  • Toto Togel
  • Situs Toto
  • AXL777
  • AERO88
  • Situs Slot Gacor
  • Situs Slot Gacor
  • Situs Toto
  • Toto Slot Gacor
  • Toto Slot
  • Toto Slot
  • DORA77
  • KOI200
  • KOI200
  • SILVAWIN
  • AXL777
  • YAMITOTO
  • NABITOTO
  • YAMITOTO
  • KOI200
  • KOI200
  • KOI200