• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

RC Kunenge aonya uvamizi mashamba Pwani,ashiriki Uzinduzi wa Bagamoyo Ardhi Klinik septr 23,2023.

Posted on: September 23rd, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Abubakari Kunenge ametoa onyo kwa wananchi wenye tabia ya kuvamia mashamba yaliyofutwa umiliki kutofanya hivyo mpaka pale Mhe. Rais atakapotoa maelekezo ya matumizi ya maeneo hayo.

Mhe. Kunenge ametoa onyo hilo aliposhiriki uzinduzi wa "Bagamoyo Ardhi Clinic" iliyofanyika katika viwanja vya Shule ya msingi Mtambani Mapinga na kuhudhuriwa na Waziri wa Ardhi Nyumba na maendeleo ya Makazi Mhe. Jery Slaa (Mb) pamoja na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Pauline Gekul (Mb).

Akizungumza katika uzinduzi huo Mhe. Kunenge ameeleza kuwa katika mkoa huo, Kata ya Mapinga ndiyo inayoongoza kwa kuwa na migogoro mingi ya ardhi na kwamba eneo hilo la mgogoro ni changamoto kubwa kwa sababu linagusa wananchi wa ngazi ya chini.

Aidha, Mhe. Kunenge ametumia fursa hiyo kumpongeza Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Mhe. Halima Okash kwa kufanya Kliniki hiyo yenye lengo la kukomesha Migogoro ya Ardhi na akaeleza matarajio yake kuwa Kata ya Mapinga iwe mfano wa maeneo korofi iliyofanikiwa katika utatuzi wa Migogoro ya Ardhi huku akiwaasa wananchi kutii na kuheshimu Sheria ili kila mtu apate haki yake.

Pia ameupongeza mhimimili wa Mahakama kwa kukubali kusikiliza Mashauri yaliyokaa muda mrefu ili kumaliza kesi hizo na akawataka wananchi kuheshimu maamuzi ya mahakama na maridhiano kwa wale watakaoridhiana nje ya Mahakama.

Kadhalika, Mhe. Kunenge ameelekeza wenye maeneo makubwa katika mkoa huo kujitokeza kushirikiana na Wakurugenzi wa Halmashauri kuyapanga maeneo hayo na kuwaletea maendeleo badala ya kuyaacha bila maendelezo.

Vilevile Mkuu huyo wa Mkoa ametumia nafasi hiyo kumueleza Waziri wa Ardhi kwamba Mkoa wa Pwani una maazimio nane ya Baraza la Mawaziri na utekelezaji wake unaendelea na kuwaelekeza wenye mtazamo tofauti kufuata utaratibu.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC Kunenge Ashiriki Kupiga Kura , Awataka Wananchi wa Pwani kuendelea kujitokeza kwa wingi

    October 29, 2025
  • Dumisheni Umoja na Utulivu kuelekea Uchaguzi Mkuu- Kamati ya Amani Pwani

    October 28, 2025
  • Vituo 3,941 vya kupiga kura vyaandaliwa Mkoani Pwani Kuelekea Uchaguzi mkuu

    October 27, 2025
  • RC Kunenge akabidhi Vitendea kazi vya Zaid ya Sh. Bilion 7 kwa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Pwani

    October 24, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.

  • Situs Toto
  • Situs Slot Gacor
  • AXL777
  • Situs Toto
  • AERO88
  • Situs Slot Gacor
  • DORA77
  • DORA77
  • DORA77
  • Toto Togel
  • Situs Toto
  • AXL777
  • AERO88
  • Situs Slot Gacor
  • Situs Slot Gacor
  • Situs Toto
  • Toto Slot Gacor
  • Toto Slot
  • Toto Slot
  • DORA77
  • KOI200
  • KOI200
  • SILVAWIN
  • AXL777
  • YAMITOTO
  • NABITOTO
  • YAMITOTO
  • KOI200
  • KOI200
  • KOI200