• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

RC Kunenge azindua kambi ya Madakati bingwa wa Mama Samia.

Posted on: June 3rd, 2024

Madaktari Bingwa wa mama Samia 45 wamepiga kambi Mkoani Pwani ,kwa siku tano kuanzia Juni 3-Juni 7 mwaka 2024 ili kutoa huduma za afya kwa magonjwa mbalimbali ikiwemo ya njia ya uzazi na watoto.

Aidha utoaji wa dawa za usingizi upasuaji wa kibobezi, magonjwa ya kawaida na kutoa rufaa kwa wale watakaohitajika.

Akizungumza Leo Juni 3 ,2024 na madaktari bingwa hao katika ukumbi wa mikutano wa mkuu wa Mkoa, Mkuu wa mkoa wa Pwani alhaj Abubakar Kunenge alieleza udaktari ni kazi ya wito na kujitolea kuokoa maisha ya watu .

Aliwataka madaktari hao kutoa huduma bora kwani wameaminiwa na ni kazi iliyobeba maisha ya watu.

Kunenge alitoa rai,kwa wataalam wa afya na madaktari kwenda na mabadiliko ya kidunia kwa kuwa wabunifu na watafiti ili kupanua uelewa na kutoa huduma bora na Kwa utaalamu zaidi.

Alimshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuboresha sekta ya afya,kuongeza vifaa tiba ,madawa na miundombinu ili kutoa huduma bora kwa watanzania .

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Pwani (RMO)Dkt.Benedicto Ngaiza alisema,wamejipanga na walianza maandalizi ya ujio huo tangu wiki iliyopita.

"Hamasa ni kubwa, tunatarajia wananchi wengi watajitokeza kupatiwa huduma na kupata tiba stahiki"

Ofisa mradi kutoka wizara ya afya, John Meena alifafanua, kampeni hiyo ya madaktari wa Samia kutoa huduma kwa wananchi ni zoezi Endelevu.

Mkoa wa Pwani una wilaya saba, Halmashauri Tisa, ina jumla ya Hospital 13 kati ya hizo Rufaa ya Mkoa Tumbi, vituo vya afya 50, kliniki za kutoa Huduma za kujifungulia 22 na zahanati 388.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC Kunenge Ashiriki Kupiga Kura , Awataka Wananchi wa Pwani kuendelea kujitokeza kwa wingi

    October 29, 2025
  • Dumisheni Umoja na Utulivu kuelekea Uchaguzi Mkuu- Kamati ya Amani Pwani

    October 28, 2025
  • Vituo 3,941 vya kupiga kura vyaandaliwa Mkoani Pwani Kuelekea Uchaguzi mkuu

    October 27, 2025
  • RC Kunenge akabidhi Vitendea kazi vya Zaid ya Sh. Bilion 7 kwa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Pwani

    October 24, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.