• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • TasksMIS |
    • Events Portal |
Coast Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Pwani

Serikali sasa kuajiri Watumishi elfu 13 Afya

Posted on: November 30th, 2023

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa kibali cha kuajiri watumishi elfu 13 katika sekta ya afya ili wapangiwe kufanya kazi kwenye vituo vya kutolea huduma hiyo kote nchini.

Hayo yamebainishwa leo Novemba 30, 2023 na Waziri wa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa - TAMISEMI ambaye ni Mbunge wa Rufiji Mohamed Mchengerwa wakati akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya chama cha Mapinduzi - CCM mbele ya viongozi wa chama hicho na wananchi kwenye viwanja vya Ujamaa Ikwiriri, Rufiji.

"Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ameendelea kuto ajira kwenye sekta ya afya na Rufiji imeendelea kupokea maafisa afya katika maeneno mbalimbali na hivi karibuni ameshatoa kibali cha kuajiri maafaisa afya, waganga (madaktari) takribani elfu 13, watakapoajiriwa, watapangiwa kazi kwenye vituo vyote vilivyojengwa wakati wa awamu ya sita kote nchini" amesema.

Mchengerwa ametoa taarifa ya kibali hicho cha Rais alipokuwa akifafanua maendeleo ya sekta ya afya kwenye Jimbo lake la Rufiji ambapo amesema kuwa katika kipindi cha 2021 hadi 2023 vituo vya afya vimeongezeka kutoka vinne hadi sita, Zahanati zimeongezeka kutoka 23 hadi 30 na akaongeza kuwa pamoja na mambo mengine, wamekamilisha ujenzi wa Jengo la Wagonjwa wa Dharura ikiwa ni pamoja na kukamilisha ujenzi wa jengo la Mionzi katika Hospitali ya Wilaya na vyote hivyo tayari vimeanza kutoa huduma kwa wana Rufiji.

"Tunaishukuru Serikali, kwani katika kipindi cha kuanzia Mwezi Julai, 2023 hadi Oktoba, 2023 tayari Sekta ya Afya imepokea jumla ya Shilingi 1,438,848,000.00 ambazo zimeanza kutekeleza miradi ya Ukarabati wa Miundombinu ya Hospitali ya Wilaya, Ukamilishaji wa Zahanati na Ujenzi wa Zahanati Mpya, Ujenzi wa Matundu ya vyoo na Miundombinu yake na Ukamilishaji wa Jengo la Wodi ya Wazazi, ameeleza.

Mchengerwa ameongeza kuwa vifaa tiba vimepelekwa katika vituo vyote vya afya na kuwa pamoja na uwepo wa Hospitali ya wilaya, kiasi cha sh. Bil. 10 kimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya kisasa itakayotoa huduma za kupokea na kuhudumia wagonjwa watakaokuwa wakipata rufaa kutoka kwenye vituo vingine vya afya wilayani humo.

Mchengerwa pia ameongelea maendeleo katika sekta za elimu, maji, miundombinu, kilimo na huduma za kijamii, uwezeshaji wananchi kiuchumi ikiwa ni pamoja na ujenzi wa masoko ya kisasa na maeneo mengine mbalimbali.

"Sisi Rufiji tunakiri kabisa, katika mambo ambayo tulilazimika kuyafanya makubwa ni kuwaahidi watanzania wa Rufiji kwamba tunaweza kubadilisha maisha yao katika mambo yanayowakera, tulipata tabu kwa miaka mingi ya nyuma katika sekta mbalimbali, sikuwa na sababu kwanini nisifanye kazi usiku na mchana kubadilisha maisha yao, watanzania wa Rufiji kwa miaka mingi wametamani maendeleo," amesema.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC Kunenge Ashiriki Kupiga Kura , Awataka Wananchi wa Pwani kuendelea kujitokeza kwa wingi

    October 29, 2025
  • Dumisheni Umoja na Utulivu kuelekea Uchaguzi Mkuu- Kamati ya Amani Pwani

    October 28, 2025
  • Vituo 3,941 vya kupiga kura vyaandaliwa Mkoani Pwani Kuelekea Uchaguzi mkuu

    October 27, 2025
  • RC Kunenge akabidhi Vitendea kazi vya Zaid ya Sh. Bilion 7 kwa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Pwani

    October 24, 2025
  • Tazama Zote

Video

Coast Region Investment opportunities
Video Nyingine

Kurasa za Haraka

  • Maswali yaulizwayo mara kwa mara
  • Hotuba za Mkuu wa Mkoa
  • Mpango Mkakati wa Mkoa
  • Investment Opportunity Profile
  • Taarifa mbalimbali kuhusu Mkoa
  • Maktaba ya Picha
  • Barua pepe za watumishi

Tovuti Zinazoshahabiana

  • OR-TAMISEMI
  • OR - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wakala ya serikali Mtandao
  • Wizara ya Elimu
  • Baraza la Mitihani la Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Visitors Counter

Location Map

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani

    Sanduku la Posta: 30080 Kibaha

    Simu ya Mezani: 023 2402287/2402500

    Simu ya Mkononi: 023 2402287/2402500

    Barua pepe: barua@pwani.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani. Haki zote zimehifadhiwa.

  • Situs Toto
  • Situs Slot Gacor
  • AXL777
  • Situs Toto
  • AERO88
  • Situs Slot Gacor
  • DORA77
  • DORA77
  • DORA77
  • Toto Togel
  • Situs Toto
  • AXL777
  • AERO88
  • Situs Slot Gacor
  • Situs Slot Gacor
  • Situs Toto
  • Toto Slot Gacor
  • Toto Slot
  • Toto Slot
  • DORA77
  • KOI200
  • KOI200
  • SILVAWIN
  • AXL777
  • YAMITOTO
  • NABITOTO
  • YAMITOTO
  • KOI200
  • KOI200
  • KOI200